Monday, January 16, 2017

EL HADARY MBIONI KUWEKA HISTORIA AFCON.

SIKU mbili baada ya kusheherekea miaka 44 ya kuzaliwa kwake, kipa wa timu ya taifa ya Misri Essam El Hadary sasa anatarajia kuweka rekodi mpya ya kuwa mchezaji mwenye umri mkubwa zaidi kushiriki michuano ya Mataifa ya Afrika inayoendelea huko nchini Gabon. El Hadary anacheza fainali zake za saba za michuano hiyo, akizidiwa moja na nguli wa zamani wa Cameroon Rigobert Song. Kipa huyo anatarajiwa kuwepo katika kikosi cha Misri kitakachokwaana na Mali katika mchezo wa kundi D utakaochezwa huko Port Gentil kesho. Kama El Hadary akipangwa katika mchezo huo atakuwa ameifunika rekodi ya Hossam Hassan aliyoweka katika michuano ya mwaka 2006 ambapo alikuwa na umri wa miaka 39.

No comments:

Post a Comment