Saturday, January 14, 2017

COSTA AACHWA KIKOSI CHA CHELSEA.

MSHAMBULIAJI wa Chelsea, Diego Costa ameachwa katika kikosi cha timu hiyo kitakachokwaana na Leicester City baadae leo kufuatia mgogoro na kocha wake juu ya siha yake. Nyota huyo wa kimataifa wa Hispania hajafanya mazoezi kwa siku tatu na ameachwa katika kikosi cha timu hiyo kilichosafiri kwenda kukwaana na mabingwa hao wa Uingereza. Taarifa hizo zimekuja kufuatia tetesi kuwa ametengewa ofa nono kwenda China ambayo itamfanya kulipwa kitita cha paundi milioni 30 kwa mwaka. Costa mwenye umri wa miaka 28 amefunga mabao 14 na kutengeneza mengine matano msimu huu. Chelsea wenyewe walikanusha taarifa hizo zilizozagaa.

No comments:

Post a Comment