Thursday, January 19, 2017

NILIKATAA KUJIUNGA NA LYON KWASABABU YA AFCON.

MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Togo, Emmanuel Adebayor amedai kuwa alikataa uhamisho wa kwenda Lyon ili aweze kuitumikia nchi yake katika michuano ya Mataifa ya Afrika. Adebayor ambaye bila klabu toka alipoondoka Crystal Palace mwishoni mwa msimu uliopita, ndio nahodha wa Togo katika michuano hiyo inayoendelea nchini Gabon. Mshambuliaji huyo angekosa zaidi ya mwezi mmoja msimu wa Ligue 1 kama Togo watafanikiwa kufika fainali Februari 5 na Lyon hawakufurahishwa na suala hilo ndio maana uhamisho wake ukashindikana. Adebayor amesema alikataa ofa ya mkataba ya Lyon ili aweze kuiwakilisha nchi yake kwani moja ya msharti katika mkataba huo ilikuwa ni kutoshiriki michuano hiyo.

No comments:

Post a Comment