Thursday, January 19, 2017

SIMEONE APOZA TAARIFA ZA GRIEZMANN KUWANIA MAN UNITED.

KOCHA wa Atletico Madrid, Diego Simeone hajashangazwa na taarifa za Antoine Griezmann kuwaniwa na klabu nyingi ikiwemo Manchester United na kuongeza kuwa hatamzuia mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Ufaransa kama akiamua kuondoka. Mapema wiki hii kumekuwa na taarifa kuwa mazungumzo kwa ajili ya nyota huyo kwenda Old Trafford yamefikia pazuri na United wanajiandaa kutoa kitita cha euro milioni 100 ili kuvunja mkataba wake na Atletico. Akizungumzia kuhusiana na taarifa hizo Simeone amesema hana mpango wa kuzuia mchezaji yeyote kwani anachofanya yeye ni kufanya kazi kwa ajili ya manufaa ya klabu. Simeone aliendelea kudai kuwa Griezmann amekuwa katika kiwnago cha juu huku akifunga mabao hivyo ni kawaida kwa klabu kubwa kumuwania.

No comments:

Post a Comment