Tuesday, January 17, 2017

SAGNA ALIMWA FAINI KWA UJUMBE ALIOTUMA INSTAGRAM.

CHAMA cha Soka cha Uingereza-FA kimemlima faini ya paundi 40,000 beki wa Manchester City Bacary Sagna kwa ujumbe wake aliotuma katika mtandao wa kijamii akihoji uwezo wa mwamuzi Lee mason katika ushindi wa mabao 2-1 waliopata katika Ligi Kuu dhidi ya Burnley mapema mwezi huu. City walipata ushindi huo kwa mabao yaliyofungwa na Gael Clichy na Sergio Aguero pamoja na kucheza wakiwa pungufu baada ya Fernandinho kulimwa kadi nyekundu kwa kumchezea vibaya Johann Gudmundsson. Katika ujumbe wake aliotuma katika mtandao wa Instagram, Sagna alindika kuwa walicheza 10 dhidi ya 12 lakini bado walipambana na kushinda mchezo kama timu. Baadae nyota huyo wa kimataifa wa Ufaransa alirekebisha ujumbe wake huo kwa kuondoka maneno ya 10 kwa 12 lakini bado FA waliamua kumlima adhabu kwa kukiuka sheria zake.

No comments:

Post a Comment