Tuesday, January 17, 2017

USAJILI WA JUVENTUS UNATOSHA - NEDVED.

MAKAMU wa rais wa Juventus, Pavel Nedved amedai kuwa hadhani kama klabu hiyo itafanya usajili mwingine katika kipindi cha usajili wa dirisha dogo la Januari. Mabingwa hao wa Serie A waliongeza nguvu katika safu yao ya kiungo kwa kumsajili Tomas Rincon kutoka Genoa, wakati pia walimsajili Mattia Caldara ambaye atabakia kwa mkopo Atalanta mpaka mwishoni mwa msimu wa 2017-2018. Nedved amesema kwasasa waemridhishwa na kikosi walichonacho hivyo itakuwa hatihati kuongeza mchezaji mwingine katika kipindi hiki. Nedved aliendelea kudai kuwa siku zote wamekuwa wakiangalia hali waliyonayo sasa na pia baadae ndio maana anaamini hawahitaji kuongeza mchezaji mwingine. Juventus kwasasa ndio wanaongoza msimamo wa Serie A wakitofautiana na AS Roma kwa alama moja.

No comments:

Post a Comment