Tuesday, January 17, 2017

UNITED YAMUONGEZA VALENCIA MWAKA MMOJA ZAIDI.

WINGA wa Manchester United Antonio Valencia amesaini mkataba mwingine wa mwaka mmoja zaidi ambayo utamuweka Old Trafford mpaka Juni 2018. Wiki iliyopita klabu hiyo ilitangaza kumuongeza mkataba Marouane Fellaini kwa miezi 12 zaidi na sasa Valencia amefuata nyayo hizo leo. Nyota huyo wa kimataifa wa Ecuador alijiunga na United akitokea Wigan Athletic mwaka 2009 na kufanikiwa kucheza mechi 271 na kufunga mabao 21.

No comments:

Post a Comment