Saturday, February 18, 2017

BELLARABI WA LEVERKUSEN AFUNGA BAO LA 50,000 BUNDESLIGA.

MSHAMBULIAJI wa Bayer Leverkusen, Karim Bellarabi amefanikiwa kufunga bao la 50,000 katika historia ya Bundesliga jana. Bellarabi alifunga bao hilo la kuongoza katika dakika ya 23 kwenye mchezo dhidi ya Augsburg likiwa ni bao lake la kwanza kwa msimu huu. Imechukua jumla ya miaka 53 kwa Bundesliga kufikia idadi hiyo ya mabao ambayo inajumuisha mabao 3,391 ya penati na mengine 984 ya kujifunga. Nguli wa Bayern Munich Gerd Muller ndio mchezaji aliyefunga mabao mengi zaidi katika ligi hiyo akiwa na mabao 365 akifuatia na Claudio Pizarro mwenye mabao 190. Katika mchezo huo Leverkusen ilishinda kwa mabao 3-1 dhidi ya Augsburg, ambapo mengine yalifungwa na Javier Hernandez.

No comments:

Post a Comment