Saturday, February 18, 2017

SPURS INAWEZA KUTWAA TAJI LA LIGI KUU.

MENEJA wa zamani wa Tottenham Hotspurs, Harry Redknapp amesema klabu hiyo itaweza kutwaa taji la Ligi Kuu ndani ya kipindi cha miaka minne. Spurs walifanikiwa kufuzu michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya kwa mara ya kwanza katika kipindi cha Redknapp na kufanikiwa kutinga hatua ya robo fainali mwaka 2011. Akizungumza na wanahabari Redknapp mwenye umri wa miaka 69 amesema Spurs wamekuwa bora chini ya Mauricio Pochettino na anadhani litakuwa kosa kubwa kumuondoa kocha huyo kwasasa. Redknapp aliendelea kudai kuwa kama Spurs ikiachwa kama ilivyo anadhani katika kipindi cha miaka mitatu au minne inaweza kutwaa taji la ligi.

No comments:

Post a Comment