Saturday, February 18, 2017

FECAFOOT YAKANUSHA BROOS KUOMBA KIBARUA AFRIKA KUSINI.

SHIRIKISHO la Soka la Cameroon-Fecafoot limekanusha taarifa kuwa kocha wao aliyewawezesha kutwaa taji la Mataifa ya Afrika mapema mwezi huu, amekuwa na mawasiliano na viongozi wa Afrika Kusini. Mapema juzi Shirikisho la Soka la Afrika Kusini-SAFA lilimtaja Hugo Broos miongoni mwa majina yaliyotuma maombi ya kibarua cha kuinoa timu ya taifa ya nchi hiyo. Katika taarifa yao Fecafoot wamedai kuwa hakuna mawasiliano yeyote yaliyofanyika kati ya Broos na SAFA mpaka sasa. Taarifa hiyo iliendelea kudai kuwa Broos amekuwa akipata ofa kadhaa baada ya michuano hiyo lakini hakuna yoyote waliyoitilia maanani kwani kocha huyo bado ana mkataba nao.

No comments:

Post a Comment