Saturday, February 18, 2017

SINA MPANGO WA KURUDI BARCELONA - GUARDIOLA.

MENEJA wa Manchester City, Pep Guardiola amesema hatarajii kurejea tena Barcelona kufuatia kuibuka mjadala wa mustakabali wa meneja wa sasa Luis Enrique baada ya timu hiyo kufanya vibaya. Enrique anatarajiwa kumaliza mkataba wake Camp Nou mwishoni mwa msim huu na nafasi ya kuondoka imeongezeka baada ya kupoteza mchezo dhidi ya Paris Saint-Germain Jumanne iliyopita. Matokeo hayo katika mchezo huo wa mkondo wa kwanza hatua ya 16 bora yanaiweka Barcelona katika hatari ya kutolewa kwenye michuano hiyo. Guardiola ambaye ameshinda mataji 14 katika kipindi cha miaka minne alikaa Barcelona amesema hana mpango wowote wa kurejea tena kwani kazi yake ilishakwisha.

No comments:

Post a Comment