Saturday, February 18, 2017

BARCELONA INAWEZA KUBADILI MATOKEO - SUAREZ.

MSHAMBULIAJI wa Barcelona, Luis Suarez anaamini kikosi chao kinaweza kuweka historia kwa kuwa wa kwanza kubadili matokeo ya kufungwa mabao mabao manne katika mchezo wa kwa mkondo wa kwanz wa Ligi ya Mabingwa Ulaya pindi watakaporudiana na Paris Saint-Germain Camp Nou Machi 8. Barcelona walichabangwa mabao 4-0 na mabingwa hao wa Ufaransa katika mchezo huo wa hatua ya 16 bora Jumanne iliyopita na kumfanya meneja Luis Enrique kukosolewa vikali. Akizungumza na wanahabari, Suarez amesema ni vigumu kupoteza mchezo kwa idadi kubwa ya mabao lakini anakiamini kikosi chao kinaweza kubadili matokeo hayo. Suarez aliendelea kudai kuwa anafahamu itakuwa changamoto kubwa kwao lakini anaamini kwa kikosi walichonacho wanaweza kubadili chochote kama wakicheza kwa kiwango chao cha juu.

No comments:

Post a Comment