Monday, February 20, 2017

WALIOFANYA VURUGU PORT SAID WAHUKUMIWA ADHABU YA KIFO RASMI.

MAHAKAMA nchini Misri imeunga mkono adhabu za kifo dhidi ya watu 10 waliohukumiwa kufuatia vurugu zilizoua watu 74 uwanjani huko Port Said mwaka 2012. Uamuzi huo wa mahakama ya Cassation ambao ndio wa mwisho, umemuondoa mshitakiwa wa 11 ambaye hakukamatwa baada ya adhabu yake ya kifo pia kuthibitishwa na mahakama nyingine June mwaka 2015. Mahakam hiyo pia imeunga mkono kifungo cha maisha kwa watu 10 na miaka mitano kwa watu wengine 12 akiwemo ofisa wa usalama wa wakati huo wa Port Said. Uamuzi huo wa mahakama umepokelewa kwa shangwe na ndugu wa watu waliopoteza maisha katika vurugu hizo, ambao walionekana nje ya mahakama wakishangilia.

No comments:

Post a Comment