Monday, February 20, 2017

DANI ALVES AWAPONDA BARCELONA.

BEKI wa zamani wa Barcelona, Dani Alves amewaponda mabingwa hao wa La Liga kwa kutompa heshima aliyostahili kabla ya kuondoka kuelekea Juventus mwaka jana. Nyota huyo wa kimataifa wa Brazil ametwaa maaji 23 katika msimu nane aliyokaa Camp Nou lakini aliondoka kama mchezaji huru na kujiunga na mabingwa hao wa Serie A mwaka jana. Akizungmza na wanahabari kuhusiana na hilo, Alves amesema katika kipindi cha msimu mitatu ya mwisho alikuwa akisikia tetesi za yeye kuondoka lakini uongozi hawakumwambi lolote. Alves aliendelea kudai kuwa Barcelona hawakumuheshimu kwnai walimpa ofa ya mkataba mpya baada ya kufungiwa kusajili na Shirikisho la Soka Duniani-FIFA. Beki huyo amesema watu wanaoongoza Barcelona hajui namna na kuwajali wachezaji.

No comments:

Post a Comment