Monday, February 20, 2017

NYOTA WA CAMEROON ATIMIKIA CHINA.

KIUNGO wa kimataifa wa Cameroon, Christian Bassogog amejiunga na klabu ya Henan Jianye ya China akitokea Aab Fodbold ya Denmark. Mapema mwezi huu, nyota huyo mwenye umri wa miaka 21 aliteuliwa kuwa mchezaji bora wa mashindano kufuatia Cameroon kutwaa taji la tano la michuano ya Mataifa ya Afrika huko gabon. Klabu ya AaB ilithibitisha taarifa hizo kupitia tovuti yao huku Bassogog mwenyewe akidai alipewa ofa ambayo hawezi kuikataa. Bassogog amesema toka alipowasili kwa mara ya kwanza Aab amekuwa akifanyiwa vyema na kila mtu ndani na nje ya uwanja hivyo anawashukuru wote waliompa ushirikiano.

No comments:

Post a Comment