Monday, February 20, 2017

BARTOMEU AWAKATA MAINI MASHABIKI WALIOMZOMEA ENRIQUE.

RAIS wa Barcelona, Josep Maria Bartomeu amesema klabu hiyo inamuunga mkono Luis Enrique kwa asilimia 100. Bartomeu amesema hakuna mpango wowote mwingine kama meneja huyo akiamua kutoongeza mkataba wake wakati utakapomalizika Juni mwaka huu. Kipigo cha mabao 4-0 walichopata Barcelona nyumbani kwa Paris Saint-Germain katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya wiki iliyopita, kimezua tetesi kuwa Enrique hataweza kuinoa klabu hiyo kwa msimu mwingine. Jorge Sampaoli na Ernesto Valverde tayari wametajwa kama makocha mabao wanaweza kuchukua nafasi kama Enrique akiondoka. Hata hivyo, Bartomeu amebainisha kuwa hawana mpango wowote mbadala kwasasa kwani kipaumbele chao ni kuhakikisha na wanafanya vizuri katika mechi zote zilizobakia msimu huu.

No comments:

Post a Comment