Monday, February 20, 2017

RUFANI YA NEYMAR YAKATALIWA.

MAHAKAMA ya Jinai ya Hispania imetupilia mbali rufani ya Neymar hivyo kumaanisha kuwa nyota huyo atalazimika kusimama kizimbani kujibu mashitaka dhidi ya tuhuma za rushwa zinazomkabili kutokana na uhamisho wake kutoka Santos kwenda Barcelona. Uhamisho wa nyota huyo wa kimataifa wa Brazil kwenda La Liga ulileta utata katika klabu hiyo huku Neymar, baba yake, rais wa zamani Sandro Rosell na rais wa sasa Josep Maria Bartomeu wote wakihusishwa na tuhuma hizo. Kesi hiyo iliibuliwa na kampuni moja ya Brazil ambao walidai kuwa walimnyimwa mgao wao wa asilimia 40 ya ada ya Barcelona waliyolipa kwa ajili ya nyota huyo, ambapo walidai hawakupata yote kama mkataba ulivyosema. Neymar alikata rufani kuhsuiana na kesi hiyo lakini mahakama imetupilia mbali rufani hiyo.

No comments:

Post a Comment