Tuesday, February 21, 2017

NIGERIA KUMUUNGA MKONO MPINZANI HAYATOU UCHAGUZI CAF.

SHIRIKISHO la Soka la Nigeria-NFF litamuunga mkono mpinzani wa rais wa sasa wa Shirikisho la Soka la Afrika-CAF, Issa Hayatou katika uchanguzi ujao. Hayatou anatarajiwa kugombea kipindi cha nane lakini anakabiliwa na upinzani kutoka kwa rais wa Shirikisho la Soka la Madagascar, Ahmad Ahmad. Rais wa NFF Amaju Pinnick amesema anadhani CAF inahitaji kizazi kipya cha uongozi ili kusogeza mbele zaidi soka la bara hili. Pinnick aliendelea kudai kuwa ataendelea kufanya kazi na Hayatou kama akishinda uchaguzi lakini kwa upande wake anaona mabadiliko yanahitaji na mtu sahihi ni Ahmad. CAF inatarajia kufanya uchaguzi mkuu Machi mwaka huu huko Ethiopia.

No comments:

Post a Comment