Tuesday, February 21, 2017

CLATTENBURG KUONDOKA MWISHONI MWA MSIMU.

MWAMUZI wa Ligi Kuu Mark Clattenburg anatarajiwa kuendelea na kibarua chake mpaka mwishoni mwa msimu huu. Clattenburg mwenye umri wa miaka 41, anatarajiwa kuwa mkuu wa waamuzi nchini Saudi Arabia na alitegemewa kuondoka mara moja. Hata hivyo, Ligi Kuu imethibitisha kuwa mwamuzi huyo anatarajiwa kusimamia mchezo wa Jumamosi hii kati ya West Bromwich Albion na Bournemouth katika Uwanja wa The Hawthorns. Clattenburg amekuwa mwamuzi wa Shirikisho la Soka Duniani-FIFA toka mwaka 2006, huku akitajwa kama mmoja wa waamuzi bora duniani kwasasa. Mwaka jana alichezesha fainali tatu za michuano ya Kombe la FA, Euro 2016 na Ligi ya Mabingwa Ulaya.

No comments:

Post a Comment