Tuesday, February 21, 2017

GUARDIOLA AWASIHI NYOTA WAKE.

MENEJA wa Manchester City, Pep Guardiola anataka wachezaji wake wahimili matarajio ya mchezo wao wa hatua ya 16 bora ya michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Monaco licha ya kuwa anafahamu watakosolewa sana kama wakishindwa kufuzu. Meneja huyo wa zamani wa Barcelona na Bayern Munich amewahi kushinda taji la michuano hiyo mara mbili akiwa kocha na hajawahi kushindwa kufuzu nusu fainali katika mara saba alizojaribu. Akizungumza na wanahabari Guardiola amesema sio kazi rahisi kuwa hapo na anataka kuwashawishi wachezaji wake kufurahia wakati huo kwnai ni mzuri. Guardiola aliendelea kudai kuwa watu wanaweza kudhani City walitakiwa kuwa hapo lakini wanasahau kuwa klabu nyingi kubwa hazipo. Meneja huuyo amesema macho na masikio duniani kote yanawatizama na kuwachambua huku wakiwaponda kama wakifungwa na kufasifia kama wakishinda.

No comments:

Post a Comment