Tuesday, February 21, 2017

ROONEY AREJEA MAZOEZINI.

MSHAMBULIAJI wa Manchester United, Wayne Rooney amerejea mazoezini kuelekea mchezo wao wa marudiano dhidi ya Saint-Etienne Jumatano ijayo. Nahodha huyo wa United amekuwa nje ya uwanja kwa kile meneja Jose Mourinho alichodai majeruhi madogo ya msuli, yaliyosababisha kukosa mchezo wa mkondo wa kwanza wa michuano hiyo pamoja na ule ya Kombe la FA dhidi ya Blackburn Rovers. Mourinho amesisitiza Rooney anaweza asiwe fiti kwa ajili ya mchezo wa marudiano dhidi ya Saint-Etienne kwasababu ya kushindwa kufanya mazoezi na kikosi cha kwanza huku pia kukiwa na hatihati ya kukosa fainali ya EFL dhidi ya Southampton Jumapili hii. Lakini nyota huyo wa kimataifa wa Uingereza alirejea mazoezini mapema leo akifanya mazoezi na wenzake wengine tisa akiwemo Chris Smalling, Marcus Rashford na Henrikh Mkhitaryan.

No comments:

Post a Comment