Wednesday, February 22, 2017

CANAVARO AKIRI TIANJIN KUFANYA MAZUNGUMZO NA ROONEY.

MENEJA wa klabu ya Tianjin Quanjian ya China, Fabio Canavaro amethibitisha kuwa timu hiyo ilishafanya mazungumzo na Wayne Rooney lakini amedai hawana mpango wowote wa kendelea na mpango huo kwasababu hatafiti aina yao ya uchezaji. Nahodha huyo wa Manchester United mwenye umri wa miaka 31, alikuwa akihusishwa na tetesi za kwenda China na vyombo vya habari vya Uingereza na kumekuwa na taarifa kuwa uhamisho wake unaweza kukamilika kabla ya muda wa mwisho Februari 28. Canavaro amesema klabu ilifanya mazungumzo na Rooney pamoja na mshambuliaji Borussia Dortmund Pierre-Emerick Aubameyang ambaye alikuwa na tetesi za kwenda Shanghai SIPG kwa kitita cha euro milioni 150 mwezi uliopita, lakini dili zote hizo hazipo mezani kwasasa. Meneja huyo aliendelea kudai kuwa kwa Rooney dili lilishindikana kutokana na nyota huyo kutokidhi kiwango cha aina ya uchezaji wao huku kwa upande wa Aubameyang wakikataliwa ofa yao na Dortmund. Tianjin walimsajili Alexandre Paton a Axel Witsel mwezi uliopita.

No comments:

Post a Comment