Wednesday, February 22, 2017

UEFA YAZIWEKA TIMU ZA REDBULL NJIA PANDA.

TAARIFA zinadai kuwa Shirikisho la Soka la Ulaya-UEFA linatarajia kuruhusu klabu moja pekee kati ya Red Bull Salzburg na RB Leipzig kushiriki katika michuano ya aidha Ligi ya Mabingwa Ulaya au Europa League. Sheria za UEFA zinaeleza kuwa haitawezekana kwa klabu mbili inayomilikiwa na mdhamini, shirika au mtu mmoja, zitakazoweza kucheza michuano hiyo kwa pamoja. Kiwango kikubwa kilichoonyeshwa na RB Leipzig iliyoanzishwa mwaka 2009 katika Bundesliga msimu huu wakifukuzia ubingwa na wakongwe Bayern Munich kumetoa picha ya wazi kuwa wanaweza michuano ya Ulaya msimu ujao. Kwa upande wa klabu ya Red Bull Salzburg ambao nao kama ilivyo kwa RB Leipzig nao wanadhaminiwa na kampuni ya vinywaji ya Red Bull, pia wako katika nafasi nzuri ya kutwaa taji la ligi la Austria ambalo litawapa tiketi ya kufuzu michuano Ulaya. Hata hivyo, moja kati ya klabu hizo italazimika kujitoa ili kuepuka kukiuka sheria za UEFA.

No comments:

Post a Comment