Wednesday, February 22, 2017

RANIERI AKITAKA KIKOSI CHAKE KUWA NA UTHUBUTU.

MENEJA wa Leicester City, Claudio Ranieri ametaka wachezaji katika kikosi chake kucheza kwa kiwango kikubwa ili kubadili upepo katika mchezo wao wa Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Sevilla. Leicester wako alama moja juu ya eneo la kushuka daraja katika Ligi Kuu baada ya kucheza mechi 25. Kutokana na kufanya hovyo katika ligi, michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya ndio imekuwa pekee waliyofanya vyema msimu huu baada ya kutinga hatua ya 16 bora wakiwa vinara wa kundi lilijumuisha timu za FC Porto, FC Copenhagen na Club Brugge. Kufuatia mchezo wao huo dhidi ya Sevilla baadae leo, Ranieri amewataka wachezaji wake kuwa na uthubutu na kucheza kwa kiwango chao cha juu.

No comments:

Post a Comment