Wednesday, February 22, 2017

LIVERPOOL MBIONI KUUHAMA UWANJA WAO WA MAZOEZI WA MELWOOD.

KLABU ya Liverpool imetangaza mipango yake mapema leo ambayo itashuhudia kikosi chao cha kwanza kikiachana na eneo lao la kipindi kirefu la mazoezi la Melwood na kuhamia eneo jipya lililoboreshwa la Kirkby ambako ndipo akademi yao ilipo. Melwood limekuwa eneo la mazoezi kwa wachezaji kadhaa wenye majina makubwa Uingereza toka mwaka 1950, akiwemo Kenny Dalglish, Ian Rush, Robbie Fowler, John Barnes na Steven Gerrard. 
Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa katika tovuti ya klabu hiyo, kama mpango huo ukipitishwa eneo la Melwood sasa litabadilishwa na kujengwa nyuma zipatazo 160. Ofisa mkuu wa mipango wa Liverpool, Andy Hughes amesema wanafahamu Melwood imekuwa eneo muhimu katika mafanikio na historia kubwa ya klabu hiyo. Hughes aliendelea kudai kuwa hata hivyo, eneo hilo kwasasa limekuwa dogo kulingana na mipango yao ya muda mrefu waliyokuwa nayo ndio maana wameamua kuhama na kuliendeleza kwa shughuli nyingine.

No comments:

Post a Comment