Wednesday, February 22, 2017

DEMBELE KUENDELEA KUBAKI CELTIC.

WAKALA wa Moussa Dembele amedai kuwa nyota huyo amepanga kukataa ofa kutoka klabu kubwa Ulaya ili aweze kubaki Celtic kumalizia mkataba wake wa miaka minne. Real Madrid ndio klabu kubwa iliyotajwa hivi karibuni kumuwania Dembele ambaye amefunga mabao 27 katika mashindano yote toka ajiunge nao akitokea Fulham Juni mwaka jana. Hata hivyo, wakala wake Mamadi Fifana amesisitiza nyota huyo wa kimataifa wa Ufaransa bado anaatka kuendelea kuitumikia Celtic. Fifana amesema Dembele alisaini mkataba wa miaka minne hivi karibuni na amepanga kubakia hapo kwa kipindi chote hicho.

No comments:

Post a Comment