Friday, February 24, 2017

KOMBE LA DUNIA 2022 LITAACHA KUMBUKUMBU YA KUDUMU - INFANTINO.

RAIS wa Shirikisho la Soka Duniani-FIFA, Gianni Infantino ana uhakika kuwa michuano ya Kombe la Dunia mwaka 2022 ambayo itaandaliwa nchini Qatar itaacha kumbukumbu ya kudumu. Infantino yuko jijini Doha kwa ajili ya Mkutano Mkuu wa Soka ambapo kamati ya maandalizi itawasilisha mipango yake kwa ajili ya michuano hiyo. Kombe la Dunia 2022 inatarajiwa kuwa ya michuano ya mwisho kuandaliwa kwa mfumo wa sasa kama mpango wa kuongeza idadi ya washiriki kutoka 32 mpaka 48 ukipitishwa. Akizungumza na wanahabari Infantino amesema lolote litakalotokea michuano hiyo itaacha kumbukumbu ya kudumu kwasababu itafanyika Mashariki ya Kati huku ikiwa mara ya kwanza kwa nchi ya kiarabu kuwa mwenyeji. Infantino aliendelea kudai kuwa pia itakuwa mara ya kwanza michuano hiyo kuandaliwa katika majira tofauti na ilivyozoeleka jambo ambalo linayafanya kuwa ya kipekee. Rais huyo amesema michuano hiyo ya Qatar pia itakuwa muhimu kwa mashabiki kwani umbali kutoka uwanja mmoja kwenda mwingine ni chini ya saa moja.

No comments:

Post a Comment