Friday, February 24, 2017

KUTIMULIWA KWA RANIERI KWAZUA GUMZO.

MSHAMBULIAJI wa zamani wa Leicester City, Gary Lineker amesema uamuzi wa klabu hiyo kumtimua Claudio Ranieri miezi tisa baada ya kutwaa taji la Ligi Kuu, ni wa kutosamehewa. Ranieri aliiongoza klabu hiyo kutwaa taji la ligi msimu wa 2015-2016 pamoja na kupewa nafasi finyu sana ya kufanya hivyo. Leicester kwasasa inashikilia nafasi ya 17 katika msimamo wa Ligi Kuu huku wakitolewa katika Kombe la FA na timu ya daraja la kwanza ya Millwall. Lineker ambaye aliwahi kuichezea Leicester kwa kipindi cha misimu saba, amesema baada ya yote Ranieri aliyoifanyia klabu hiyo anadhani kumtimua ni jambo lisilokubalika. Naye meneja wa zamani wa Tottenham Hotspurs, Harry Redknapp amesema hajashangazwa sana na uamuzi huo ili amesikitika kwani alifanya kazi yake vyema.

No comments:

Post a Comment