Thursday, February 16, 2017

CLATTENBURG KUIKACHA LIGI KUU.

CHAMA cha Makocha wa Kulipwa-PGMOL kimetangaza kuwa mwamuzi Mark Clattenburg anatarajiwa kuondoka Ligi Kuu ya Uingereza na kujiunga na Shirikisho la Soka la Saudi Arabia-SAFF. Clattenburg katika miezi ya karibuni amekuwa akihusishwa na tetesi kadhaa baada ya kukiri kuwa anaweza kuondoka kama ilivyo kwa wachezaji kadhaa nyota wa Ulaya walioondoka Uingereza kufuatia ofa nono walizopewa China. Badala yake mwamuzi huyo ameamua kwenda kwenye taifa hilo la kiarabu lenye utajiri mkubwa katika soka ingawa haijathibitishwa rasmi kibarua gani haswa atapewa huko. Mwamuzi mwezake wa zamani wa Ligi kuu Howard Webb alikuwa ameteuliwa kama mkubwa wa waamuzi wa SAFF Agosti mwaka 2015 lakini mapema mwezi huu alijiuzulu kufuatia kukubali kwenda kuwa msimamizi mkuu wa shughuli za mfumo mpya wa teknologia ya video kwa ajili ya kusaidia waamuzi huko Marekani.

No comments:

Post a Comment