Thursday, February 16, 2017

RAIS WA ZAMANI WA BARCELONA AMLAUMU BARTOMEU KUKIMBIA KIVULI CHAKE.

RAIS wa zamani wa Barcelona, Joan Laporta amemtuhumu rais wa sasa wa klabu hiyo Josep Maria Bartomeu kujificha kufuatia kipigo kikubwa cha fedheha walichopata kutoka kwa Paris Saint-Germain-PSG kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya. Barcelona walitandikwa mabao 4-0 katika Uwanja wa Parc des Princes mabao ambayo yaliwekwa kimiani na Angel Di Maria na Julian Draxler kwenye mchezo huo wa mkondo wa kwanza hatua ya 16 bora. Laporta amesema kuwa Bartomeu alitakiwa kujitokeza baada ya kipigo hicho na kukubali lawama kwa aibu hiyo waliyopata Barcelona. Laporta aliendelea kudai kuwa anafahamu kama rais lazima ujisikie vibaya na alitegemea hatua ya kwanza ambayo angechukua Bartomeu ni kujitokeza na kuzungumzia sauala hilo lakini hajamuona mahali popote. Bartomeu alichukua mikoba ya kuiongoza Barcelona Januari mwaka 2014 kufuatia kujizulu kwa Sandro Rosell na toka wakati huo klabu hiyo imefanikiwa kutwaa taji la La Liga mara mbili, Kombe la Mfalme mara mbili na moja la Ligi ya Mabingwa Ulaya.

No comments:

Post a Comment