Thursday, February 16, 2017

INFANTINO ATAKA MWENYE ZAIDI YA MMOJA KOMBE LA DUNIA 2026.

RAIS wa Shirikisho la Soka Duniani-FIFA Gianni Infantino amesema amepanga kuhamasisha mwenyeji zaidi ya mmoja katika Kombe la Dunia 2026 kwani michuano hiyo inaweza kugawanywa kwa nchi mpaka nne. Akizungumza na wanahabari mapema leo, Infantino amesema wanatarajia kuhamasisha kuwepo mwenyeji zaidi ya mmoja katika Kombe la Dunia kwasababu FIFA inataka kuonyesha ina busara na kufikiria mipango endelevu ya muda mrefu. Infantino aliendelea kudai kuwa wanaweza kujumuisha pamoja nchi mbili, tatu au nne ambazo zinaweza kuja na mpango wa viwanja vitatu, vinne ay vitano kila moja ili kupunguza gharama na nchi hizo zinapaswa kuwa zimepakana. Hatua hiyo inakuja kufuatia wasiwasi juu ya gharama kubwa zinazotumika michuano hiyo ikiandaliwa na nchi moja na baadae viwanja vilivyojengwa kwa fedha nyingi kutelekezwa. Michuano ya Kombe la Dunia imewahi kuandaliwa kwa ushirikiano wa nchi mbili mara moja pekee nayo ilikuwa mwaka 2002 Japan na Korea Kusini.

No comments:

Post a Comment