Thursday, February 16, 2017

HATMA YA WENGER KUJULIKANA MWISHONI MWA MSIMU.

UAMUZI wa mustakabali wa meneja wa Arsenal, Arsene Wenger unatarajiwa kufanyika mwishoni mwa msimu huu lakini ofa ya mkataba mpya kwa kocha huyo bado iko mezani. Pamoja na kipigo kizito walichoapata katika mchezo wa mkondo wa kwanza wa 16 bora ya michuano ya Ligi ya Mabingwa jana kutoka Bayern Munich, hakuna dalili zozote za meneja huyo kutimuliwa kabla ya kumalizika kwa msimu. Inategemewa uamuzi wa kubakia au kuondoka unatarajiwa kufanyika kwa maelewano kati ya klabu na meneja huyo Mfaransa mwenye umri wa miaka 67. Wenger amekuwa meneja wa Arsenal toka mwaka 1996, na mapema msimu huu alipewa ofa ya mkataba mpya.

No comments:

Post a Comment