Tuesday, February 14, 2017

MAJERUHI YAMKOSESHA LUKAKU KAMBI DUBAI.

MSHAMBULIAJI wa Everton, Romelu Lukaku anatarajiwa kukosa kambi ya mazoezi huko Dubai kwasababu ya kupatiwa matibabu ya majeruhi ya mguu. Klabu hiyo ilitangaza kuwa nyota huyo mwenye umri wa miaka 23 anatarajiwa kwenda nchi kwao Ubelgiji kumuona daktari ili kushughulikia tatizo lake. Hata hivyo, Everton wana uhakika majeruhi ya Lukaku sio makubwa sana na anatarajiwa kuwa fiti kwa ajili ya mchezo wao ujao wa Ligi kuu dhidi ya Sunderland Februari 25 mwaka huu. Mchezaji mwingine pekee aliyekosa safari hiyo ni Yannick Bolasie ambaye amekuwa nje ya uwanja kwa kipindi kirefu akisumbuliwa na majeruhi ya goti. Lukaku amekua katika kiwango bora msimu huu kufuatia kufunga mabao 16 katika mechi 24 za ligi alizocheza.

No comments:

Post a Comment