Tuesday, February 14, 2017

RIBERY, BOATENG KUIKOSA ARSENAL KESHO.

KLABU ya Bayern Munich inatarajiwa kuwa bila winga wake Franck Ribery na beki wa kati Jerome Boateng katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Arsenal utakaofanyika kesho. Bayern walikuwa na matumaini wawili wangeweza kurejea kwa wakati kwa ajili ya mchezo huo wa mkondo wa kwanza hatua ya 16 bora utakaofanyika katika Uwanja wa Allianz Arena. Hata hivyo, inavyoonekana Ancelotti atawakosa nyota wake hao kufuatia Ribery kuwa bado anafanya mazoezi peke yake. Ribery amekuwa katika kiwango bora msimu huu akisaidia kutoa pasi za mwisho katika mechi dhidi ya Freiburg na baadae Werder Bremen kwenye ushindi wa mabao 2-1 waliopata katika mechi hizo Januari. Boateng yeye bado anaendelea kujiuguza bega lake ambalo liliteguka mwishoni mwa mwaka jana.

No comments:

Post a Comment