Tuesday, February 14, 2017

GUARDIOLA AMUOMBEA JESUS.

MENEJA wa Manchester City Pep Guardiola ana matumaini kuwa mshambuliaji wake Gabriel Jesus hakupata majeruhi makubwa ya mguu katika ushindi wa mabao 2-0 waliopata kwenye mchezo wa Ligi Kuu dhidi ya Bournemouth. Jesus mwenye umri wa miaka 19 amefunga bao katika mechi zake mbili za kwanza za ligi alizoanza lakini alijikuta akicheza dakika 14 pekee katika mchezo huo wa jana baada ya kuteguka kifundo cha mguu katika Uwanja wa Vitality. City wanatarajiwa kujua ukubwa wa tatizo alilopata Jesus baada ya kufanyiwa vipimo zaidi. Jesus ambaye alitua City akitokea Palmeiras Januari mwaka huu, alifunga bao katika ushindi waliopata dhidi ya West Ham United na Swansea City na alikuwa akitaka kuweka rekodi ya kuwa mchezaji wa tatu wa klabu hiyo baada ya Emmanuel Adebayor na Kevin de Bruyne kufunga bao katika mechi zao tatu za kwanza za ligi.

No comments:

Post a Comment