Tuesday, February 14, 2017

BARCELONA KUFANYA USAJILI WA DHARULA KUZIBA NAFASI YA VIDAL.

MENEJA wa Barcelona, Luis Enrique amethibitisha kuwa Barcelona wanaangalia uwezekano wa kusajili beki mpya wa kulia baada ya Aleix Vidal kukosekana kwa msimu wote uliobakia. Vidal ambaye amekuwa katika kiwango kizuri toka kuanza mwaka huu aliteguka kifundo chake cha mguu katika ushindi waliopata dhidi ya Alaves Jumamosi iliyopita na anatarajiwa kukaa nje kwa miezi mitano. Kuumia huko kwa Vidal kunamuacha Sergi Roberto kuwa mchezaji pekee katika klabu hiyo anayecheza nafasi hiyo kwasasa. Dirisha la usajili kwasasa limeshafungwa, lakini kwa sheria za Hispania Barcelona wanaweza kuruhusiwa kufanya usajili wa dharula ili kuziba nafasi iliyo wazi. Akizungumza na wanahabari, Enrique amesema Vidal tayari ameshaanza matibabu na sasa wanaangalia uwezekano wa kusajili mchezaji mwingine kwasaabu sheria zinawaruhusu. Barcelona wanatarajiwa kuvaana na Paris Saint-Germain katika mchezo wao wa mkondo wa kwanza wa hatua ya 16 bora ya michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya utakaochezwa huko Parc de Princes.

No comments:

Post a Comment