Sunday, February 12, 2017

KLOPP ADAI TIMU YEYOTE INGEM-MISS MANE.

MENEJA wa Liverpool, Jurgen Klopp anaamini kila timu duniani ingeyumba bila Sadio Mane baada ya nyota huyo wa kimataifa wa Senegal kufunga mabao mawili katika ushindi wa mabao 2-0 waliopata dhidi ya Tottenham Hotspurs jana. Mane alirejea kutoka katika majukumu ya kimataifa akiwa na Senegal na kufunga mabao hayo ambayo yameipa Liverpool ushindi wa kwanza kwa mwaka huu. Akizungumza na wanahabari Klopp amesema walikuwa wakihitaji mtu wa mwisho ambaye anafunga na Mane alifanya vyema katika mchezo huo. Klopp aliendelea kudai kuwa waliyumba kumkosa Mane Januari lakini kila timu duniani ingekuwa kama hivyo kwa kumkosa nyota huyo.

No comments:

Post a Comment