Sunday, February 12, 2017

MWAMUZI BORA CLATTENBURG AIOMBA RADHI HULL CITY KWA BAO LA SANCHEZ.

BEKI wa Hull City, Andy Robertson amesema mwamuzi Mark Clattenburg amewaomba radhi kwa kuruhusu bao lenye utata la Alexis Sanchez lililoipa ushindi Arsenal wa mabao 2-0. Nyota huyo wa kimataifa wa Chile alionekana wazi akitumbukiza mpira wavuni kwa mkono katika dakika ya 34 kwenye mchezo huo uliofanyika katika Uwanja wa Emirates kabla ya kufunga bao lingine kwa penati dakika za nyongeza. Akizungumza na wanahabari, Robertson amesema ni kweli sanchez alikuwa ameshika na wakati wakitoka katika vyumba wakati wa mapumziko mwamuzi aliwaomba radhi na kukiri halikustahili kuwa bao. Robertson aliendelea kudai kuwa kilikuwa kitendo cha haraka sana hivyo huwezi kumlaumu mwamuzi moja kwa moja. Naye meneja wa Arsenal, Arsene Wenger amesema baada ya mchezo pamoja na mwmauzi kufanya makosa kwa Hull lakini pia hata kwa upande wao mwamuzi alifanya maamuzi yaliwaumiza.

No comments:

Post a Comment