Sunday, February 12, 2017

LUCA TONI APONDA WALIOSHAMBULIA GARI AKIWA NA RAIS WA VERONA.

MSHAMBULIAJI wa zamani wa kimataifa wa Italia, Luca Toni amewaponda mashabiki walioshambulia gari lao akiwa na rais wa Verona Maurizio Setti wakati wakiwa njiani kuelekea kuangalia mchezo wa Serie B dhidi ya Avellino. Toni ambaye amewahi kuichezea Verona kwa misimu mitatu amedai kuwa gari lao lilivamiwa na watu 15 huku kioo cha upande mmoja wa gari kikidaiwa kuvunjwa. Toni na Setti walikuwa wakielekea katika Uwanja wa Partenio kwa ajili ya mchezo huo ambao Verone walifungw amabao 2-0, na nguli huyo wa zamani wa Bayern Munich na Juventus alikosoa vikali tukio hilo walilofanyiwa. Akihojiwa na Sky Sport, Toni ambaye alikuwa sehemu ya kikosi cha Italia kilichotwaa Kombe la Dunia mwaka 2006, amesema Setti alikuwa amevaa skafu ya bluu hivyo anadhani mashabiki hao walidhani ni watu wa kawaida na hawakuwajua.

No comments:

Post a Comment