Sunday, February 12, 2017

MOURINHO ADAI HASIFIWI INAVYOSTAHIKI.

MENEJA wa Manchester United, Jose Mourinho amedai juhudi za safu yake ya ushambuliaji zingepongezwa zaidi kama mtu mwingine ndio angekuwa akiinoa klabu hiyo. United ilitawala mchezo kwa kiasi kikubwa hatua iliyowafanya kupata ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Watford ambayo yaliwekwa kimiani na Juan Mata na Antony Martial. Akizungumza na wanahabari, Mourinho aliwapongeza wachezaji wake kwa kiwango bora walichoonyesha na kuongeza kuwa kama angekuwa kocha mwingine lazima angepewa pongezi za juu kuliko yeye. United pamoja na kuendelea kubaki katika nafasi ya sita lakini nyuma ya alama moja kufikia eneo la kufuzu michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya.

No comments:

Post a Comment