Sunday, February 12, 2017

KNTE ANAFAA KUTWAA TUZO YA MCHEZAJI WA MWAKA - HENRY.

NGULI wa zamani wa soka wa Ufaransa, Thierry Henry amempigia chapuo kiungo wa Chelsea N’Golo Kante kutwaa tuzo ya mchezaji bora wa mwaka wa PFA baada ya kuonyesha kiwango bora toka atue Stamford Bridge. Nyota huyo wa kimataifa wa Ufaransa ambaye aliisaidia Leicester City kutwaa taji la ligi msimu uliopita alihama King Power na kutua Chelsea kiangazi mwaka jana. Henry amesema wiki iliyopita alikwenda kwenye mazoezi ya Chelsea kumuona Eden Hazard lakini alikutana na Kante na kumgusa huku akimuuliza kama kweli ni yeye na kumfanya acheke. Henry aliendelea kudai kuwa kutokana na kiwango kikubwa anachokionyesha Kante haoni sababu kwanini asishinde tuzo hiyo.

No comments:

Post a Comment