Sunday, February 12, 2017

SINA MPANGO WA KUONDOKA ARSENAL - WENGER.

MENEJA wa Arsenal, Arsene Wenger amesisitiza hana mpango wa kuondoka Arsenal pamoja na Ian Wright kudai kuwa kocha huyo yuko mbioni kuondoka. Mustakabali wa Wenger umekuwa ukihojiwa kufuatia vipigo mfululizo katika mechi dhidi ya Watford na Chelsea vilivyofanya kufifisha matumaini yao ya ubingwa. Hata hivyo, Arsenal ilirejesha makali yake kufuatia ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Hull City mapema jana. Akizungumza na wanahabari waliohoji mustakabali wake baada ya mchezo huo, Wenger alibainisha kuwa bado ataendelea kuinoa klabu hiyo na hajafikiria suala la kuondoka kwasasa. Wenger aliendelea kudai kuwa jambo la muhimu kwasasa ni kuhakikisha wanshinda mechi zao halafu baada ya msimu kumalizika ndio wanaweza kujadili mustakabali wake.

No comments:

Post a Comment