Friday, February 10, 2017

KLOPP AWAPOZA MASHABIKI WA LIVERPOOL.

MENEJA wa Liverpool, Jurgen Klopp bado ana uhakika kazi yake ni mpango wa muda mrefu, kueleka katika mchezo wao wa Ligi Kuu dhidi ya Tottenham Hotspurs Jumamosi hii. Liverpool imekuwa katika kiwango duni hivi karibuni wakiwa wamefanikiwa kupata ushindi katika mechi moja kati ya 10 walizocheza toka kuanza kwa mwaka huu. Kipigo cha hivi karibuni kilitoka kwa Hull City mwishoni mwa wiki iliyopita ambapo Klopp baadae alikubali lawama kwa kushuka kiwango cha timu hiyo. Liverpool sasa inashikilia nafasi ya tano katika msimamo wa ligi wakiwa nyuma ya vinara Chelsea kwa alama 13. Akizungumza na wanahabari Klopp amesema bado anaamini mipango yake ni ya muda mrefu na anafahamu kuwa jukumu lake ni kuwaongoza wachezaji katika njia sahihi.

No comments:

Post a Comment