Friday, February 10, 2017

CONTE ADAI UNITED WAKO KWENYE MBIO ZA UBINGWA.

MENEJA wa Chelsea, Antonio Conte amesisitiza kuwa Manchester United bado wako katika mbio za ubingwa pamoja na kuwazidi kwa alama 14. United tayari wameshacheza mechi 15 mfululizo bila kufungwa katika Ligi Kuu lakini bado wameendelea kubakia nafasi ya sita katika msimamo wkiwa alama mbili nyuma ya Arsenal waliopo nafasi ya nne. Akizungumza na wanahabari, Conte amesema kuna timu sita imara na zinaweza kupigana kushinda taji. Conte aliendelea kudai kuwa United bado wana nafasi ya kutwaa ubingwa pamoja na pengo kubwa la alama lililopo kati yao.

No comments:

Post a Comment