Friday, February 10, 2017

MKHITARYAN AMSHUKURU KLOPP.

KIUNGO wa Manchester United, Henrikh Mkhitaryan amemshukuru Jurgen Klopp kwa ushauri uliomsaidia kupita mwanzo mgumu alipotua Old Trafford. Klopp alikuwa akimpa ushauri mchezaji huyo kwenye kipindi kigumu wakati walipokuwa katika klabu ya Borussia Dortmund mwaka 2013. Mapema msimu huu, Mkhitaryan hakucheza mechi yeyote ya ligi kwa wiki 10 na alikumbuka ushauri aliokuwa akipatiwa na Klopp. Akizungumza na wana habari, nyota huyo alimshukuru Klopp kwa kumsaidia kwa kiasi kikubwa kisoka na hata ushauri. Nyota huyo wa kimataifa wa Armenia alifanya kazi na Klopp kwa misimu miwili Ujerumani kabla ya meneja huyo hajajiuzulu na baadae kutua Liverpool Octoba mwaka 2015.

No comments:

Post a Comment