Friday, February 10, 2017

DELLE ALLI, KOCHA WA SWANSEA WATWAA TUZO YA MWEZI.

KIUNGO wa Tottenham Hotspurs, Dele Alli amefanikiwa kutwaa tuzo ya mchezaji bora wa mwezi Januari akimshinda mchezaji mwenzake wa timu hiyo Harry Kane. Alli na Kane kila mmoja amefunga mabao matano katika mechi za ligi Januari na kuisaidia Spurs kutofungwa katika mechi tano wakishinda mechi dhidi ya Watford, Chelsea na West Bromwich Albion huku wakitoa sare na Manchester City na Sunderland. Beki wa kulia wa Everton Seamus Coleman naye pia alikuwepo katika kinyang’anyiro hicho kufuatia kuisaidia timu yake kutofungwa katika mechi tatu za ligi walizocheza Januari. Kwa upande mwingine meneja mpya wa Swansea City Paul Clement yeye ametwaa tuzo ya kocha bora wa mwezi baada ya kushinda mechi tatu kati ya nne alizosimamia mwezi uliopita. Clement aliteuliwa kuchukua kibarua hicho Januari 3 na kuisaidia kuichapa Crystal Palace mabao 2-1 katika siku yake ya kwanza kazini kabla ya kuja kufungwa na Arsenal mabao 4-0 na baadae kkushinda tena mechi dhidi ya Liverpool na Southampton.

No comments:

Post a Comment