Friday, February 10, 2017

CARROLL AMSHINDA GIROUD BAO BORA LA MWEZI.

MSHAMBULIAJI nyota wa Crystal Palace, Andy Carroll amefanikiwa kutwaa tuzo ya bao bora la mwezi akimshinda nyota wa Arsenal, Olivier Giroud katika kinyang’anyiro hicho. Januari mosi Giroud alifanikiwa kufunga bao murua lililopewa jina la Scorpion kick katika mchezo dhidi ya Palace hatua ambayo ilidhaniwa ndio linaweza kuwa bao la mwezi. Hata hivyo, Palace ilifanikiwa kujibu mapigo kwa bao safi la Carroll alilofunga katika dakika ya 79 ya mchezo dhidi ya West Ham United katika Uwanja wa London Januari 14. Akizungumza na wanahabari Carroll amefurahi kushinda tuzo hiyo haswa ikizingatiwa kuwepo kwa mabao mengine mazuri yaliyofungwa mwezi uliopita.

No comments:

Post a Comment