Friday, February 10, 2017

MARADONA AKUBALI KUWA BALOZI WA FIFA.

NGULI wa soka wa Argentina, Diego Maradona amethibitisha kukubali kuwa balozi wa Shirikisho la Soka Duniani-FIFA na kueleza furaha yake ya kujiunga na shirikisho hilo safi na linalofanya shughuli zake kwa uwazi. Maradona mwenye umri wa miaka 56 ambaye amewahi kutwaa Kombe la Dunia akiwa na Argentina mwaka 1986, alikuwa mpinzani mkubwa wa rais wa zamani Sepp Blatter aliyeondoka kufuatia kashfa kubwa ya ufisadi iliyolikumba shirikisho hilo mwaka 2015. Maradona alituma picha katika ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa Facebook akiwa pamoja na rais wa sasa Gianni Infantino, na kusema sasa atatimiza ndoto yake aliyokuwa kwa kipindi kirefu. Maradoma amesema sasa anaweza kutimiza ndoto yake ya kufanya kazi kwa usafi na uwazi na FIFA sambamba na watu ambao wanaolipenda soka na kuwashukuru wote waliomuunga mkono katika changamoto hiyo mpya.

No comments:

Post a Comment