Friday, February 10, 2017

MOURINHO ALITAKA KUMPELEKA WILLIAN MAN U.

WINGA wa Chelsea, Willian amebainisha kuwa Manchester United ilitaka kumsajili katika kipindi cha majira ya kiangazi. Nyota huyo wa kimataifa wa Brazil amekuwa hana nafasi ya moja kwa moja katika kikosi cha kwanza msimu huu, huku akibadilishana na Pedro mara kwa mara. Willian mwenye umri wa miaka 28 alikuwa mchezaji muhimu katika kikosi cha Chelsea kilichotwaa taji chini ya Jose Mourinho miaka miwili iliyopita. Willian amekiri kuwepo kwa maombi kutoka United na kufafanua kuwa ni kwasababu Jose Mourinho yuko kule.

No comments:

Post a Comment