Friday, February 10, 2017

SUAREZ KUKOSA FAINALI YA KOMBE LA MFALME.

MSHAMBULIAJI wa Barcelona, Luis Suarez anatarajiwa kukosa mchezo wa fainali ya Kombe la Mfalme Mei 27 baada ya kushindwa rufani kupinga kadi ya pili ya njano aliyopewa katika mchezo dhidi ya Atletico Madrid Jumanne iliyopita. Shirikisho la Soka la Hispania-RFEF limetoa adhabu ya kumfungia mechi mbili Suarez kutokana na tukio lake baada ya kutolewa nje katika dakika za mwisho katika mchezo huo uliomalizika kwa sare ya bao 1-1. Baada ya rufani hiyo kukataliwa, Barcelona wamesema sasa watakwenda mbali zaidi kwenye kamati ya rufani ya RFEF ili kujaribu tena kuipinga kadi hiyo. Suarez alisema baada ya mchezo kuwa uamuzi wa kadi hiyo ulikuwa wa kuchekesha na kuitaka klabu kukata rufani jambo ambalo meneja Luis Enrique alifanya.

No comments:

Post a Comment